Sunday, September 20, 2015

kwanini glass huweza kupasuka ikiwekewa maji ya moto (WHY DOES GLASS BREAK WHEN POURED WITH HOT WATER)

glass huweza kupasuka ikiwekewa kimiminika cha moto kwa sababu kuu moja, glass inapowekewa kitu cha moto, mabadiliko hayo ya jotoridi hupokelewa na upande wa ndani wa glass, joto hilo husababisha upande huo wa glass kutanuka, endapo upande wa nje wa glass utatanuka kwa uwiano wenye tofauti kubwa na ule wa ndani basi nyufa huweza kutokea kwenye glass hiyo, na hatimaye kupasuka kabisa.
Vivyo hivyo maji ya baridi sana huweza kupasua glass endapo mabadiliko ya jotoridi la ndani ya glass yatatofautiana na ya nje kwa uwiano mkubwa, yaani kusinyaa kwa glass upande wa ndani utatofautiana sana na upande wa nje.

NINI KIFANYIKE KUZUIA HI
1. Mimina maji au kimiminika chako taratibu ili kuifanya glass iendane na jotoridi la kiminika hicho, hii itasaidia kuepukana na tatizo la kupasuka kwa glass yako
2. Pia kwa kimiminika cha moto glass yaweza kupashwa moto kwa kuiweka sehemu yenye digrii 40-50 za jotoridi

UNAWEZA JIFUNZA KITU KINGINE PIA HAPO
Hata katika maisha ya kawaida ya binadamu, kupokea mabadiliko yoyote, ni lazima uwe umejiandaa kuyapokea, na mabadiliko yoyote yale kwa mtu yanaanzia kwake, yaani moyoni mwake, ukiwa tayari kubadilika wewe ndipo mtu mwingine anaweza kukuletea mabadiliko.
CHANGE NI WEWE.

Thursday, September 17, 2015

majina ya waliokosa vyuo (wanaotakiwa kuomba kwa mara nyingine 2015?2016)

Click link hii kuangalia majina ya wanaotakiwa kuomba kwa mara nyingine kujiunga na vyuo vikuu 2015/2016. Hii ni baada ya kukosa nafasi katika maombi yao ya kwanza.
 Kwa herufi kati ya A-H
http://www.tcu.go.tz/images/pdf/Group%20(A_H).pdf
  Kwa herufi kati ya I-L
http://www.tcu.go.tz/images/pdf/Group%20(I_L).pdf
 Kwa herufi kati ya M-N
http://www.tcu.go.tz/images/pdf/Group%20(M_N).pdf
 Kwa herufi kati ya O-Z
http://www.tcu.go.tz/images/pdf/Gruop%20(O_Z).pdf

Sunday, September 13, 2015

wanafunzi wa shule ya sekondari Ngudu wafurahia huduma ya maji ya bomba


 
hali ilivyokua kabla ya huduma ya maji kusogezwa karibu 

Shule ya Ngudu iliyopo wilayani kwimba ni moja ya shule iliyokumbana na tatizo la ukosefu wa walimu, pamoja na wanafunzi wake kukosa vipindi kwa muda mrefu kwa tatizo la ukosefu wa maji.
Kwa mujibu wa mhandisi wa maji wa wilaya hiyo Boaz Pius http://www.worldbank.org watu walikua wakipata maji ya bomba kwa masaa matatu mpaka manne kwa siku na wakati mwingine kutopata kabisa, walikuwa wakitegemea maji ya visima sita vilivyochimbwa na waingereza miaka ya 1950.
lakini kwa sasa serikali kwa msaada wa world bank wameweza kuwaletea maji ya bomba eneo hilo.
huduma hiyo imesaidia kwani mwanzo hata watoto wa shule ya sekondari Ngudu na walimu walilazimika kukatisha vipindi kutokana na ukosefu huo wa maji laini kwa sasa hawapati usumbufu huo tena.
wananchi wa eneo hilo wameufurahia mradi huo ulioanza kwa idadi ya makazi yapatayo 700 kuunganishwa na huduma hiyo ya maji,
kupitia mradi wa kahama shinyanga water supply authority KASHYWASA.
 
HALI ILIVO SASA